Partners implementing the EEVT project

Partners implementing the EEVT project

Project Profile

The EEVT Project is implemented by the Vocational Education Training Authority (VETA) and international development charity VSO, in partnership with BG Tanzania. The EEVT project (Enhancing Employability through Vocational Training) aims at improving the employability of young people in the regions of Mtwara and Lindi, with a focus on the growing demand for skilled labour in the gas industry and related services. Over 2 years, VETA teachers and their students will be trained by tutors from VSO. On the long run, VETA will be capable of producing a steady stream of qualified craftsmen and teachers.

More than 620 students from VETA Mtwara and more than 224 students from VETA Lindi are benefiting from the project. The number of students benefiting from the project will continue to increase as more students continue to join for both short and long courses while others graduating as from 2014. 4 Teachers from VETA Lindi and 7 VETA Mtwara are also part of beneficiaries in this project through capacity building (training by City and Guilds) and also one-on one coaching from VSO technical advisors.

The EEVT project is governed by the signed memorandum of understanding (MOU) which among other things stipulates the role of each partner to the project. GIZ, VETA, VSO Tanzania and Tanzania LNG have signed the MOU which provides the framework of all operations and project activities
in a model of partnership approach. On 10th October 2013, the three partners have also signed another MOU for EEVT VETA Lindi extension in the presence of Hon. First Lady Mama Salma Kikwete who was the Guest of Honour during inauguration of the project in Lindi. Prior the Lindi inauguration, the same project was also inaugurated in November 2012 by Hon. Dr. Mohamed Gharib
Bilal at VETA Mtwara. The project steering committee, with membership representation from GIZ, VETA, Tanzania LNG and VSO Tanzania, is the top overseer and decisive body of the project.

Since 2014, the project has scaled up in terms of support and recognition where more extractive companies have joined their forces to support the project. Currently, the project is supported by GIZ and Tanzania LNG Plant Project - a joint venture combined of 5 major O&G companies (BG Group, Ophir, Pavilion Energy, ExxonMobil and Statoil). The first phase of the project ended in December 2015 (2012-2015) and the second was extended for the next 2 years from January 2016 to December 2017.

Among the notable and key components covered in phase includes industry Links program, Capacity of Centers, Quality of Training, International Accreditation and Career Matching. These five components form the basis of EEVT phase two project where a block system approach will be introduced and placing industry links at the core of the project. In addition, phase two has added three new trades based on the experience of phase one; scaffolding, plant operator and industrial painting of which the training is expected to be provided in short course basis.


Ijumaa, 25 Oktoba 2013

SPEECH BY MAMA SALMA KIKWETE DURING INAUGURATION OF EEVT GAS & OIL RELATED OPPORTUNITY PROJECT AT VETA LINDI


 
HOTUBA YA MKE WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
MHESHIMIWA
MAMA SALMA KIKWETE
 
 
 
AKIZINDUA MRADI WA MAFUNZO KWA SEKTA YA GESI NA MAFUTA YA PETROLI
 
 
CHUO CHA MAFUNZO NA ELIMU YA UFUNDI STADI, LINDI,
10 OKTOBA, 2013
 
 

 HOTUBA YA MKE WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA MAMA SALMA KIKWETE, AKIZINDUA MRADI WA MAFUNZO YA GESI NA MAFUTA YA PETROLI, CHUO CHA MAFUNZO NA ELIMU YA UFUNDI STADI, LINDI

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi -
Mheshimiwa Philipo Mulugo (Mb)
Mkuu wa Mkoa wa Lindi  -
Mheshimiwa Ludovick Mwananzila
Mkuu wa wilaya ya Lindi;
Mkurugenzi Mkuu VETA – Eng Zebadiah  S. Moshi
Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya ufundi – Leah Lukindo
Meneja wa Tanzania wa  British Gas – Kate Sullam
Mkurugenzi wa Tanzania wa Volunteer Service Organisation – Jean Van Wetter
Mkurugenzi wa VETA kanda ya kusini mashariki – Wilhard Soko
Wakuu wa vyuo vya VETA Lindi na Lindi  
Washirika  wengine wa Maendeleo;
Waheshimiwa Viongozi wa Vyama vya Siasa;
Waheshimiwa Wabunge;
Viongozi wa Serikali;
Viongozi wa Dini;
Waalimu;
Wageni Waalikwa;
Wanafunzi;
Mabibi na Mabwana:

Ndugu Wananchi:
Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha mahali hapa katika kutekeleza majukumu ya Kitaifa kwa jamii na hasa vijana ambao ndio kundi lengwa kwa siku ya leo.

Ninayo furaha kubwa pia kuja hapa Lindi kuzindua awamu ya pili ya Mradi wa Mafunzo na Elimu ya Ufundi Stadi kwa ajili ya Sekta ya Gesi na Mafuta ya Petroli wenye madhumuni ya kuimarisha ajira kwa vijana kupitia ufundi stadi Lindi  (Enhancing Employability through Vocational Training – EEVT).

Ninapenda kuanza kwa kutoa shukurani na pongezi zangu za dhati na kipekee kwa Kampuni ya British Gas ya Uingereza, Voluntary Services Organisation (VSO Tanzania) ya Uingereza, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, VETA, na wote walioshiriki kufanikisha kuanzishwa na kuendelezwa kwa Mradi huu. Ninapenda pia, kuwashukuru washirika wengine wa maendeleo ambao wameshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha kuanza kwa Mradi huu hususan Serikali ya Uingereza kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID), British Council, Serikali na wananchi wa Mkoa wa Lindi .  

 Naipongeza pia Bodi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi chini ya  Mwenyekiti wake Prof. Idrissa Bilal Mshoro pamoja na Menejimenti ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inayoongozwa na Eng. Zebadiah Moshi, kwa kuhamasisha uanzishwaji wa Mradi huu na sasa tuko katika hatua ya pili ya uzinduzi wa mradi kwa mkoa wa Lindi, hongereni sana. Nina imani kubwa kuwa wataendelea kufanya kazi nzuri ili malengo ya Mradi huu yaweze kutimia. Pia, ninatambua kazi kubwa iliyofanywa katika awamu ya kwanza ya mradi huu katika chuo cha ufundi VETA Mtwara na sasa awamu ya pili kwa VETA Lindi.

 Shukurani za pekee pia ziwaendee kampuni ya British Gas ambayo imeonesha ushiriki mzuri katika kufadahili mradi huu kwa chuo hiki cha Lindi . British Gas ambao ni washirika wakuu wa mradi huu Pamoja na mchango mkubwa wa ajira kwa washiriki, makampuni ya Petroli na Gesi watapata wafanyakazi walioiva vizuri na hivyo kuongeza tija katika kazi na uzalishaji kwa vijana na jamii ya Lindi na maeneo ya jirani.

Ndugu Wananchi;
Natambua kuwa mradi kama huu tayari umeanza kwa mkoa wa Mtwara katika chuo cha ufundi VETA Mtwara ambapo Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Gharib Bilal alizindua mradi huo pale Mtwara mwishoni mwa mwaka jana 2012. Ninajisikia mwenye furaha kufanya vivyo hivyo katika uzinduzi huu kwa mkoa wa Lindi nikiamini vijana wa Lindi na maeneo mengine watafaidika na fursa hii. Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wadau wote wa maendeleo kupitia vyombo husika kama VETA ili kujenga mazingira mazuri ya kutoa ajira.

 Nimepewa taarifa kuwa mradi huu ambao utakuwa wa miaka 2 kuanzia 2013 hadi 2015  ambapo wanafunzi zaidi ya 224 watapata mafunzo toka kwa walimu wenye uzoefu wa kimataifa kwa kushirikiana na walimu wa hapa Lindi na kukifanya chuo cha ufundi stadi Lindi kuwa cha kiwango cha kimataifa. Pia mradi huu  utaboresha kozi za chuo ili ziendane na mahitaji ya soko hususani sekta ya Gesi na Mafuta.

 Katika kufanikisha hilo, nimeambiwa kuwa walimu 4 katika karakana 4 za hapa Lindi watajengewa uwezo kwa kupewa kozi zenye hadhi ya kimataifa ili wapate tuzo zinazotambulika kimataifa.  Nimefurahi sana kusikia kuwa walimu hawa 4 tayari wameanza kujengewa uwezo kwa kushirikiana na wenzao wa VETA Mtwara. Vilevile, Wataalamu wa kimataifa kutoka shirika la VSO wameanza kutoa ushauri na uzoefu wao kwa kushirikiana na walimu wetu wa hapa VETA Lindi hasa kwa kuzingitia fursa za gesi na mafuta. Mradi huu pia utaboresha matumizi ya lugha ya kiingereza kwa walimu wasiopungua 15 kwa sababu vijana wetu wanatarajiwa kuajiriwa katika makampuni ya ndani na ya kimataifa, hivyo lugha ya kiingereza nyenzo muhimu ya mawasiliano.

 Ndugu Wananchi
Ushiriki wa wananchi, utayari wao wa kumiliki maendeleo yao na kujituma kwao pamoja na uongozi na usimamizi mzuri wa Serikali ya Mkoa utakuwa ndio chachu ya mafanikio ya Mradi huu. Mradi huu utakuwa na mchango mkubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi , Mikoa ya jirani na Taifa kwa ujumla katika kuboresha hali ya maisha ya kaya kwa kuwapatia ujuzi mbalimbali katika Sekta ya Gesi na Mafuta ya Petroli, utakao wawezesha wahitimu kujiajiri au kuajiriwa.

 Ndugu Mabibi na Mabwana
Ninatoa ombi na rai kuwa makampuni mengi yajitokeze kushiriki katika mradi huu kwani una mafanikio makubwa si kwa wahitimu peke yake bali kwa makampuni pia kwani watapata wafanyakazi mahiri watakao tumia muda mfupi kuelewa wajibu wao.  Wito wangu kwa VETA ni kupanua wigo wa mashirikiano na waajiri ili tuweze kujenga nguvu kazi itakayokidhi matakwa ya soko la ajira ili tuweze kufanikiwa kufikia malengo ya mipango ya kitaifa kama Mpango wa Taifa wa miaka 5, Mkakati wa kukuuza uchumi na kupunguza umasikini awamu ya 2, Matokeo makubwa sasa (Big Result Now) na hivyo kuifikia dira ya maendeleo ya Taifa 2025 ya kuwa nchi yenye pato la kati.  Mafunzo ya ufundi Stadi katika nchi mbalimbali imekuwa chachu ya maendeleo.  Ninaahidi kuwa serikali kama inavyoyapa msisitizo mafunzo ya ufundi stadi kipaumbele, itaendelea kuijengea VETA uwezo ili iweze kumudu majukumu yake.
 
Ndugu wananchi
Kwa namna ya kipekee sana naomba nitoe msisitizo nikiwa kama mama lakini pia kama mmoja wa wana-maendeleo katika Mkoa wa Lindi. Ninatambua changamoto za mtoto wa kike katika kupata elimu kwa ngazi zote. Ni matumaini yangu kuwa fursa hii ya mradi huu itatoa mwanga kwa mtoto wa kike. Nitoe wito kwa wazazi na walezi kuwajengea mazingira mazuri watoto wa kike ili washiriki sawa na watoto wa kiume katika kunufaika na mradi huu. Wataalamu wanasema; ukimuelimisha mtoto wa kike umeelimisha jamii nzima. Tutumie fursa hii vizuri ili vijana wetu wapate ujuzi wenye viwango vya kimataifa na hivyo kushindana katika soko la ajira la sasa.

Ndugu wananchi
Nafurahi kuzindua Mradi huu nikiwa na matumaini makubwa kwamba Watanzania hasa vijana sasa tumepata moja ya ufumbuzi wa changamoto ya ajira hasa kwa vijana, kwa kutumia fursa ambazo zimejitokeza katika Sekta hii.

Ndugu wananchi na Wageni Waalikwa,
Baada ya kusema haya machache, sasa natangaza rasmi kuwa nimezindua rasmi Mradi huu wa Mafunzo na Elimu ya Ufundi Stadi kwa Sekta ya Gesi na Mafuta ya Petroli kwa chuo cha ufundi stadi Lindi.

Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni